TAG Penuel Revival Temple ni kanisa linalojikita katika Neno la Mungu, upendo na roho ya ushirika kwa wote.

"Bwana Yesu asifiwe! Ninakukaribisha kwa upendo mkuu katika hekalu la Bwana."
Mungu ameweka kusudi kubwa kwa kila mwanadamu. Hapa TAG Penuel, dhamira yetu kuu ni kuhakikisha unagundua kusudi hilo, unakua katika imani, na kuenenda katika utukufu wa Kimungu ambao amekuandalia tangu kuumbwa kwa misingi ya dunia.
Iwe unatembelea tovuti yetu kwa mara ya kwanza au unatafuta mahali pa kusali na kujenga familia yako kiroho, tunakukaribisha Jumapili hii kushiriki nasi hekalu letu lililopo Kilosa, Morogoro. Mungu akubariki sana!
Kuhubiri Injili ya Yesu Kristo kwa watu wote, kuwafundisha na kuwaimarisha waumini katika Neno, na kuwalea kiroho ili wawe wanafunzi waliokomaa na wenye ushuhuda mwema wa maisha ya Kikristo kwa utukufu wa Mungu.
Kuwa kanisa hai lenye nguvu ya Roho Mtakatifu, lililojazwa upendo, umoja, na ushuhuda thabiti unaoleta mabadiliko chanya katika jamii na kuvuta roho za watu kwenye wokovu wa kweli.
Tunathamini uaminifu katika Neno la Mungu, maisha ya utakatifu na maombi, ushirika wa dhati, ukarimu kwa jamii, uaminifu wa kifedha, na malezi ya kiroho kwa kizazi kipya.
TAG Penuel Revival Temple ilianza kama kikundi kidogo cha maombi miaka kumi iliyopita chini ya mti wa mwembe. Kwa neema ya Mungu na kujitolea kwa waumini wa kwanza, kanisa lilijenga hekalu lake la kwanza na kukua kuwa moja ya nguzo kuu za kiroho na kijamii katika eneo la Kilosa.
Leo hii, tukiwa na mamia ya waumini wanaoshiriki kila wiki, tunaendelea kusimamia misingi ile ile ya upendo wa dhati na Injili ya moto ili kugusa maisha ya watu kiroho, kiuchumi, na kijamii.
Kutana na watumishi wa Mungu wanaoongoza idara, huduma, na usimamizi wa TAG Penuel Temple.
Mchungaji Mkuu
Mchungaji kiongozi wa kanisa la Penuel Revival Temple.
Mother
Kuhamasisha kanisa katika kiroho.
Katibu wa WWK
Katibu wa WWK.
Mhasibu
Mhasibu na Mzee wa Kanisa Penuel.
Mwenyekiti wa WWK
Mwenyekiti wa idara ya WWK.
Katibu wa Kanisa
Katibu wa Kanisa.
Katibu wa CMF
Katibu wa Idara ya CMF.
Pakua fomu za uanachama, katiba ya kanisa, bulletins za kila wiki na masomo ya Biblia ya hekalu letu.
Pakua katiba rasmi ya kanisa kuelewa muundo, miongozo na taratibu zetu za kiutawala.
Fomu rasmi ya maombi ya uanachama wa kudumu katika kanisa la TAG Penuel Temple.
Kitabu cha mwongozo wa masomo ya Biblia na maswali ya majadiliano katika vikundi vya nyumbani.
Majibu mepesi kwa maswali ya kawaida kuhusu ibada zetu na jinsi ya kushiriki.